Hali hiyo inadaiwa kusababishwa na kushuka kwa kiwango cha elimu shuleni hapo.
Baadhi ya wanafunzi shuleni hapo, Peter Chambai, Hassan Saidy na Teresia John, wamekiri kufanyika kwa vitendo hivyo viovu, ambavyo wameviita ni ukatili na unyanyasaji wa kisaikolojia dhidi ya wanafunzi wasiopenda mchezo huo mchafu.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Tree of Hope, Fortunata Manyeresa, ameahidi kuingia mtaa kwa mtaa kuwasaka wanafunzi wanaojihusisha na vitendo vya ngono wakiwa na umri mdogo ili wanaowarubuni wachukuliwe hatua.