Search in This Blog

Showing posts with label CHADEMA. Show all posts
Showing posts with label CHADEMA. Show all posts

ZITTO AZIDI KUIPA TABU CHADEMA, SOMA HAPA KUJUA NI TABU GANI


HUKUMU iliyosomwa na Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, John Utumwa, Jumanne iliyopita (juzi), imemuongezea uzito Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, sasa amekuwa mzito zaidi ndani ya chama chake.

Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe akiwa ndani ya Mahakama Kuu wakati akisubiri hukumu ya kesi yake juzi.
Awali, ilionekana kama uamuzi wa Kamati Kuu (CC) ya Chadema ni msumari wa mwisho na kwamba Zitto hana uzito wowote wa kuutilia changamoto lakini kile kilichoamuliwa na mahakama ni wazi kimemuongezea nguvu mbunge huyo.
Wafuasi wa Zitto wakiwa na mabango wakati wa hukumu yake.
Hukumu ya Jaji Utumwa, ilimpa ushindi Zitto kuhusu pingamizi lake aliloweka mahakamani akitaka mahakama iweke zuio kwa CC ya chama chake kujadili uanachama wake mpaka atakapopewa fursa kukata rufaa katika Baraza Kuu la Chadema.
Kutokana na hukumu hiyo, baadhi ya wananchi walitoa maoni yao kwamba, Zitto anaweza kupumua sasa angalau kwa kiasi fulani kuweza kuuthibitishia umma kuwa, CC ilimuonea.
“Angeshindwa mahakamani, angekuwa na hatima mbaya kwenye chama chake, tena angefukuzwa uanachama mara moja lakini mahakama imempa nguvu, sasa uzito wake ni mkubwa na hata wanaomuunga mkono wanaweza kutembea kifua mbele,” alisema Shadrack Lyimo aliyekuwa mahakamani juzi.
Zitto, amefungua mashtaka mahakamani akimshitaki katibu mkuu wa chama chake na baraza la wadhamini  kwa kutompa fursa ya kuukatia rufaa uamuzi wa CC wa kumvua nyadhifa zake zote na sasa kesi ya msingi itasomwa kwa mara ya kwanza Februari 13, mwaka huu.
Katika madai ya msingi, Zitto anataka katibu mkuu na baraza la wadhamini wa Chadema kumpa fursa ya kukata rufaa Baraza Kuu kwa maelezo kwamba, CC ilikiuka taratibu ya kumvua nyadhifa zote za uongozi.
Jaji Utumwa akisoma hukumu yake alisema CC hairuhusiwi kujadili uanachama wa Zitto mpaka hukumu ya kesi ya msingi itakapotolewa au pale Baraza Kuu litakapoitishwa na kusikiliza rufaa ya mbunge huyo.

HUU NDIO MPANGO WA ZITTO KUTOTAKA KUJADILIWA UWANACHAMA WAKE


TABIA ya Mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu, kumrushia madongo Mbunge wa Kigoma Kaskazini kwa tiketi ya chama hicho, Zitto Kabwe, imesababisha hasira kwa mlengwa na sasa ameamua kuchukua uamuzi mkali zaidi.

Zitto Kabwe pamoja na Mwanasheria wake,Albert Msando (kulia) wakiwasili katika Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam jana wakiongozana na wafuasi wanaopinga kuvuliwa uongozi wake, tayari kwa kwenda kusikiliza hukumu ya kesi yake.
Zitto, ameamua kumrudi Lissu kwa staili nyingine kwa kwenda moja kwa moja na kummaliza Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kwa sababu anayo makombora mengi makali ambayo hapo kabla aliyaficha ili kunusuru chama.
Chanzo chetu kimesema, Zitto amekasirishwa na mashambulizi kutoka kwa Lissu na kwamba baada ya kukaa kimya muda mrefu, sasa uzalendo umemshinda, kwa hiyo kinachofuata ni mashambulizi mwanzo mwisho dhidi ya Mbowe.
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe.
“Huu ni mpango endelevu, Zitto anajua kwamba maneno ya Lissu ni ya kulishwa, mhusika ni Mbowe, ndiyo maana amesema hataki majibishano na kifaranga, anamtaka mama wa kifaranga ajitokeze,” alisema rafiki wa Zitto kwa sharti la kutotajwa jina na kuongeza:
“Mpango uliopo ni kukabiliana na mama wa vifaranga, yapo mabomu mengi ya maana ambayo Zitto anayo dhidi ya Mbowe, anachosubiri ni hukumu ya pingamizi lake mahakamani kuhusu Kamati Kuu ya Chadema kujadili uanachama mpaka itakampo fursa ya kukata rufaa Baraza Kuu.”
Hukumu hiyo, ilitarajiwa kusomwa jana Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam chini ya Jaji John Utamwa.

Mkurugenzi wa Sheria na Haki za Binadamu wa Chadema, Tundu Lissu.
Jumapili iliyopita, Zitto alisema kuwa maneno yanayozungumzwa na viongozi wa Chadema, mengi yakipitia kwenye kinywa cha Lissu ni sawa na mipasho kwa sababu hayamo kwenye tuhuma 11 ambazo walimwandikia azijibu kwa maandishi.
Kwa upande wa Mbowe, alinukuliwa akisema kuwa Zitto hapaswi kuibua tuhuma mpya dhidi yake, isipokuwa anachopaswa kufanya ni kujibu yale ambayo anatuhumiwa, huku akiyaita maneno ya mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini ni ya kitoto.

ZITTO KABWE AIBUKA KIDEDEA KWENYE KESI YAKE

Mahakama kuu ya kanda ya dar es salaam imempa kinga ya muda mbunge wa kigoma
Kasikazini mh. Zito kabwe  kutojadiliwa uanachama wake na kamati kuu ya chadema

HUYU NDIO MWENYEKITI WA CHADEMA ALIYEPIGWA KIPONDO USIKU WA KUAMKIA LEO NA KUTUPWA

ununio1Mwenyekiti wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wilaya ya Temeke Joseph Yona amepigwa na watu wasiojulikana na kisha kutupwa kwenye eneo la Ununio kwenye Magorofa ya Wasomali Kawe Dar es salaam.
Shuhuda Abdul Ally ambae ni mkuu wa nyumba zilizokaribu na alikopigwa Mwenyekiti huyu, anasema walisikia kelele za huyu mtu kupigwa saa tisa usiku na walipomsogelea walimkuta peke yake.
‘Niliomba wasiniue, wamenipiga sana… wamenichukua saa tano nyumbani kwangu Kwa Aziz Ally, wao walikua na gari kama ya Polisi lakini inaonekana sio ya polisi wakasema tunakupeleka Central, tulikua wanne na hawakuhangaika na mtu wakanichukua mimi moja kwa moja.. tulipopanda kwenye gari wakachukua nguo yangu wakanifunga uso, wakaanza kunipiga wakisema nisiwajibu na hawakuniambia chochote’
Unaweza kusikiliza maelezo yake mengine akihojiwa kwa kubonyeza play hapa chini..

ununio8 ununio7 ununio6 ununio5 ununio4 ununio3 ununio1 DSC_0027 ununio2

HATMA YA ZITTO KABWE CHADEMA KUJULIKANA KESHO SAA NANE



Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe.
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imeahirisha kutoa au kutotoa zuio la muda kwa Kamati Kuu ya Chadema kutojadili uanachama wa Zitto Kabwe mpaka kesho saa nane mchana!

ZITTO ASEMA YA MOYONI, NI KUHUSU UFISADI UNAOFANYWA NA FREEMAN MBOWE

Akizungumza katika press conference ya CHADEMA na waandishi wa habari iliyofanyika leo, Mwanasheria mkuu wa Chadema, Mh.Tundu Lisu alisema kuwa mkakati wa kuwachafua viongozi ni wa siku nyingi ambapo Chama kimefanikiwa kunasa mawasiliano ya Zitto tangu mwaka 2009 alipokuwa akiwasiliana  na  akina Denis Msack wa Mwananchi.

 Lissu alisema njama hizi ndio zilizopelekea mpaka mashtaka ya Ugaidi ambapo katika mahojiano yake ya Star Tv akiwa na akina Mwigulu Nchemba Zitto hakukanusha, pia aliandika kwenye mitandao kuwa Chadema imtose Wilfred Lwakatare 
 
Lissu aliongeza kuwa Zitto mpaka sasa ana magari mawili ya Nimrod Mkono na Mkono mwenyewe ndiye amewaambia taarifa hizo. Mkono amewaambia kuwa amempa Zitto hela nyingi sana na Zitto alishiriki moja kwa moja kumzuia mgombea wa Chadema katika Jimbo la Nimrod Mkono .
 
====Huu  ni  ujumbe  wa  Zitto Kabwe  kujibu  mapigo  ya  Tundu Lissu===
**
Lissu anasema nimepewa magari 2 na Mzee Mkono. Anasema kaambiwa na Mkono. Naamini Mkono alimwambia pia mwaka 2005 alimpa Freeman Aikaeli Mbowe tshs 40m ili Mbowe asifanye kampeni Musoma vijijini. 

 Nadhani alimwambia pia mwaka 2008 (baada ya orodha ya mafisadi kutangazwa 2007) Mkono alimpa Freeman tshs 20m za uchaguzi wa Tarime na Freeman akasema kwenye chama ametoa mkopo na akalipwa.

 Nadhani alimwambia pia kuwa Mwaka 2010 Mkono alimpa Mbowe tshs 200m za kampeni ya Slaa. Pia hakusahau kumwambia kuwa Rostam Aziz alimpa Mbowe tshs 100m za kampeni. Lissu anajua kuwa gazeti la Tanzania Daima limeanzishwa na fedha za chama kutoka Conservative party?

Nimefanya internship yangu kwa Mkono and Company Advocates kuhusu masuala ya mikataba. Mzee Mkono ni Mzee wangu na alisaini petition ya kumtoa Waziri Mkuu Pinda.

Lissu awaambie waliyemtuma wamwambie ukweli wote. Lissu ajue yeye ni kifaranga tu, Mimi namtaka mama wa kifaranga ajitokeze. Aeleze aliingia deal gani na Kinana na Sumaye mwaka 2005 kufuatia deni lake NSSF. Aweke wazi mkataba kati yake na NHC kuhusu nyumba ya Umma ilipo Club Bilicanas.

They must know I am not a push over. Chacha died, I won't.

Mtu ambaye hawezi kuheshimu mke wake aliyemzalia watoto hawezi kunyooshea mtu kidole kuhusu maadili.

YASOME HAPA MAAMUZI YA CHADEMA YA KAMATI KUU

Katibu Mkuu  anaanza kwa kuomba radhi kwa kuchelewa kuanza press akiungana na John Mnyika pia Katibu Mkuu anasema kuwa atasoma neno kwa neno kutokana na umuhimu wa hoja yenyewe! Ameanza kusoma na kusema kamati kuu ilikuwa ni ya dharura iliyokuwa na lengo la kuwajadili Wanachama watatu Dr. Kitila Mkumbo, Zitto Kabwe na Samsoni Mwigamba.
Dr Slaa anaonyesha kabrasha lenye nyaraka mbalimbali ikiwemo mkakati wa mabadiliko 2013, mashtka ya watuhumiwa na nyaraka nyingine muhimu. Sasa Dr. Slaa anasoma mashtaka yote 11 ya Watuhumiwa kama walivyokabidhiwa kwa maandishi

Katibu Mkuu anasema Watuhumiwa wawili yaani Dr. Kitila Mkumbo na Samsoni Mwigamba waliitikia wito wa Kamati Kuu lakini aliyehojiwa na Kamati Kuu ni Dr. Kitila Mkumbo pekee ambaye katika utetezi wao walikana kuvunja katiba ya Chama na Kanuni zake.
Katibu Mkuu anasema Dr Kitila Mkumbo alikiri kumfahamu M2 na anamjua fika lakini hawezi kumtaja mpaka awasiliane nae kwanza. Pia Dr Kitila Mkumbo alisema yeye na Mwandishi wa waraka ule walimpa briefing Mh. Zitto Kabwe kwa hiyo alikuwa anaufahamu waraka huo.


Dr. Kitila Mkumbo alikataa kuzungumzia vifungu vya katiba walivyodai vimevunjwa kwa madai kuwa tayari wana malalamiko kwa msajili tayari. Aidha Dr. Kitila Mkumbo alishindwa kuithibitishia Kamati Kuu kwa ushahidi kuhusu madai ya taarifa ya fedha ambazo yeye na Zitto walishiriki, pia alishindwa kuonyesha ushiriki wa M/Kiti katika manunuzi ya vifaa mbalimbali vya Chama zikiwemo pikipiki za Chama.

MH. TUNDU LISSU ABWAGA CHOZI..CHEZEA SIASA WEWE.

Mbunge na mwanasheria wa chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA akilia machozi ya ajabu baaada ya purukushani yiliyosababishwa na makundi yaliyokuwa yakipingana...Wanaomuunga mkono na wasiomuunga mkono Mh Zitto Kabwe...!Anayebembeleza ni mbunge wa viti maalumu CHADEMA Mh. Jocya Mukya...HATARI SANA... IMEKAAJE HII...TOA MAONI YAKO HAPO CHINI

ANGALIA FUJO ZA CHADEMA MAHAKAMANI HAPO JANA

Ni January 3 2014 asubuhi ambapo watu mbalimbali wakiwemo Wafuasi na Wanachama wa Chadema walikua wamekusanyika Mahakama kuu kanda ya 88.5 Dar es salaam wakitaka kujua kitakachotokea manake kesi ya Mbunge Zitto Kabwe dhidi ya chama chake cha Chadema ilikua inaendelea.

Muda mfupi kabla ya kuanza kusikilizwa kwa kesi hiyo, asubuhi kulitokea fujo baada ya jamaa mmoja alieshtukiwa kwamba anarekodi mazungumzo ya moja kati ya vikundi vilivyokua vimesimama kwenye kordo ya Mahakama kuanza kushambuliwa.
Yani ilikua hivi…….. wakati kesi inasubiriwa kuanza kusikilizwa kulikua na makundi mbalimbali ya hawa Wafuasi, wengine upande wa Chadema, wengine upande wa Mbunge Zitto Kabwe ambapo kwenye hivyo vikundi ndio kuna kimoja kikaanzisha vurumai baada kushtukia mchezo.
 Mpaka mwisho, hakikujulikana kilikua kikundi cha upande gani kati ya hizi pande mbili za hii kesi ambayo imeahirishwa mpaka Jumatatu January 6 2014

ZITTO AIBUKA KIDEDEADHIDI YA CHADEMA MAHAKAMANI LEO

 Aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Zitto Kabwe (kulia) akitoka katika Mahakama Kuu ya Tanzania, Dar es Salaam leo, ambapo aliwasilisha ombi la pingamizi la yeye kutojadiliwa kwenye kikao cha Kamati Kuu ya chama hicho kinachotarajia kufanyika kesho, hadi rufaa yake ya kupinga kuenguliwa wadhifa huo kwenye Baraza Kuu la chama hicho. Kushoto ni Wakili wa Zitto, Albert Msando. Mahakama Kuu imekubaliana na Zitto Kikao cha Kamati Kuu ya Chadema kinachotarajiwa kufanyika kesho kutomjadili kwa namna yoyote.
Zitto Kabwe akiingia mahakama Kuu Dar es Salaam leo
Wanasheria wa Chadema, Tundu Lisu (kushoto) na Peter Kibatala waliofika kupinga hoja hiyo mahakamani.
Tundu Lisu na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema wakijadiliana jambo wakati wakisubiri uamuzi wa mahakama
Zitto ana wakili wake Msando wakiwasiliana na marafiki zao walipokuwa wakisubili uamuzi wa mahakama, ambapo Zitto aliibuka dedea kwa pingamizi lake kukubaliwa hivyo kikao cha Kamati Kuu kinachofanyika kesho kukatazwa kumjadili kwa namna yoyote Zitto.

MH ZITTO KABWE ATINGA MAHAKAMANI, ANGALIA HAPA

Mh. Zitto Kabwe atinga Mahakamani asubuhi hii ni Baada ya Jana Kuanza kwa Kuibwaga CHADEMA iliyowakilishwa na Wakili wake Tundu Lissu.Tofauti na Jana Mh.Zitto alifika mahakamani na Usafiri wake,HIi leo Zitto ametinga Mahakamani Kwa Miguu akitokea Kempisck Hotel akiongozana na Mwanasheria Wake Alberto Mhando,Hali ya Mahakama ni Tulivu Kabisa,Watu wamejitokeza kwa Uchache sana,Team Mbowe+Team Slaa na Team ZItto Kwa uchache wao wanabadilishana Mawazo,hakuna mkwaruzo wowote ule hapa Mahakamani.

Picha za ZItto akitinga Mahakamni Ingia hapa






SUMAYE AKARIBISHWA KUINGIA CHADEMA NA MBOWE

MWENYEKITI wa taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe amemkaribisha Waziri Mkuu mstaafu Fredrick Sumaye kujiunga na chama chake ili kuendeleza mapambano dhidi ya vitendo vya rushwa.

Mbowe alitoa kauli hiyo hivi karibuni wakati wa sherehe za ufunguzi wa jengo jipya la ibada zilizofanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheli Usharika wa Lole Mwika na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali na kanisa ambapo Sumaye alikuwa mgeni rasmi.

Alisema hoja ya rushwa inayozungumzwa na Sumaye ambayo CHADEMA imekuwa mstari wa mbele kuipiga vita ina msingi, hivyo viongozi wengine wanapaswa kumuunga mkono na kuliomba kanisa lizidi kuwaombea viongozi wa aina hiyo ili wazidi kupaza sauti zao bila hofu.

“Ndugu zangu hoja ya rushwa iliyozungumzwa mahali hapa na Sumaye ni hoja ya msingi sana, haki katika taifa hili ni bidhaa adimu na wale wanaotetea haki katika taifa hili wengine wanailipa kwa gharama ya maisha yao,” alisema.

Alisisitiza kuwa ni vyema viongozi wakawa na mipaka ya vyama vyao vya siasa na kuwa na lengo moja la kusimamia hatma ya taifa kwa kupigania haki bila uwoga ili kuepusha mateso kwa wananchi.

“Viongozi wote kama tukaamua kusimamia hii hoja bila ya kuona  huyu yuko chama gani, yule yuko chama gani, tukafanya hili suala la rushwa ni la taifa, basi tunaweza kupiga hatua, na kama hatutasahau mipaka ya vyama vyetu hakika nchi hii bado wananchi wa kawaida wataendelea kuteseka sana,” alisema.

Mbowe aliomba kanisa lisaidie katika suala hilo ili kuepusha taifa kupasuka kutokana na viongozi kuweka itikadi mbele na kusahau kuwa siasa ni masuala yanayopita.

Alisema hivi sasa vyama vya siasa vimetafsiriwa kama vyombo vya kugombanisha watu, huku baadhi ya viongozi kwa makusudi wakisahau kuwa vyama vya siasa ni vyombo vya uchaguzi vinavyotumika kupata viongozi.

“Tunauana kwa mabomu, tunauana kwa risasi, tunafungana kwa ajili ya siasa, siasa ni kazi ya kupita, kama Mungu amemuandika mtu kuwa na uongozi atapata uongozi bila ya kujali yuko chama gani, kwa hiyo niombe kanisa lifanye suala la uchaguzi kuwa ajenda ya kudumu ya kanisa,” alisema.

Akizungumzia mwaka mpya 2014, Mbowe alisema ni mwaka wa kutisha kwa watu ambao wapo katika siasa adhimu (active politics) wanaoona namna siasa zinavyobadilika na kuwa ni mambo ya kutishia uhai wa watu.

“Huu ni mwaka wa majaribu makubwa na tunaliomba kanisa lisikae mbali, kanisa lina wajibu mkubwa wa kutusaidia wanasiasa maana tunapokuwa ndani ya nyumba za ibada kama hizi kwa kiwango fulani tunaheshimiana,” alisema.

HATMA YA ZITTO KABWE MWAKANI


KAMATI Kuu ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), inayotarajiwa kuketi mwishoni mwa mwezi Februari mwakani, ndiyo itakayoamua hatma ya kisiasa ndani ya chama hicho kwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe.

Zitto alivuliwa wadhifa wake wa Unaibu Katibu Mkuu wa chama hicho na kamati hiyo iliyoketi kwa siku mbili kuanzia Novemba 20-21, na kumpa siku 14 za kujieleza kwanini asifukuzwe uanachama kwa tuhuma za kukihujumu, kukisaliti chama chake na viongozi wenzake.

Desemba 10, mwaka huu, Mbunge huyo wa Chadema aliwasilisha utetezi wake Makao Makuu ya Chama hicho.

Akizungumza na MTANZANIA Jumapili lililotaka kufahamu hatua ya chama ilipofikia hasa baada ya Zitto kuwasilisha utetezi wake, Katibu wa Chadema, Dk. Wilbrod Slaa alisema maamuzi dhidi ya rufaa hiyo yataamuliwa na Kamati Kuu itakayoketi kulingana na Kalenda yake.

“Iko Kamati Kuu na huko kuna taratibu zake kwani kamati hiyo haikai kwa ajili ya mtu mmoja, huko itasikilizwa na kutolewa maamuzi kulingana na kalenda yake” alisema Dk. Slaa.

Hata alipotakiwa kufafanua kuwa Kamati Kuu itakutana lini Dk Slaa hakuwa tayari kwa madai kuwa suala hilo ni kwa mujibu wa kalenda ya chama hicho.


Mtanzania  lilimtafuta msemaji wa Chadema, Tumaini Makene ambaye alisema kamati hiyo itakaa kwa mujibu wa ratiba yake iliyopo ndani ya Katiba ya Chama hicho pasipo kutaja tarehe wala mwezi.

“Kamati itakaa kwa mujibu wa Katiba, angalia ndani ya Katiba utagundua inakaa baada ya muda gani,” alisema Makene.

Kwa mujibu wa Katiba ya chama hicho, kamati kuu huwa inaketi kila baada ya miezi mitatu ndani ya mwaka.

Katika Katiba hiyo sura ya saba imeandikwa kuwa “7.7.15 Kamati Kuu itakutana mara nne (4) kwa mwaka. Vikao maalum/dharura vinaweza kuitishwa kadri itakavyolazimu kwa mujibu wa kanuni za Chama,” ilieleza.

Hivyo mkutano ujao unatarajia kuwa mwezi Februari mwishoni mwaka 2014.

Mbali na Zitto, kamati kuu hiyo ya Chadema iliyoketi katika ukumbi wa wa Ubungo Plaza, Dar es Salaam ilifikia uamuzi wa kuwavua uongozi viongozi wake wengine wawili wakihusishwa na tuhuma za usaliti wa kuandaa mpango wa kufanya mabadiliko ya uongozi ndani ya chama hicho.

Viongozi waliovuliwa uongozi kwa kuhusika na Waraka huo ni mjumbe wa Kamati Kuu pamoja na Dk Kitila Mkumbo na Samson Mwigamba aliyekuwa Mwenyekiti wa chama hicho Mkoa wa Arusha.


Mtanzania:

ROMA MKATOLIKI ANA MPANGO WA KUJIUNGA NA CHADEMA

Roma Mkatoliki akiongea na mabest zake Wa Mtaani huko Tanga amesema ana mpango Kuingia Kwenye Uringo wa Kisiasa ili apate nafasi Nzuri ya Kuikosoa Serikali baada ya Muziki wake Kupuuzwa na Viongozi wa Taifa hili.


Naplan Kuzamia Kwenye Mambo ya Politics hivi sasa, By the Way Wiki Ijayo naweza Kuchukua Kadi ya Chadema Rasmi”… Pia amesema Atahakikisha Wasanii Wenzake wanaoimba Muziki wa HipHop akina Kala Jeremiah nao Wanaunda timu ya Maangamizi Kuing’oa CCM Madarakani, ila aliwasihi sana Viongozi wa Chadema Kuwa Karibu nao pale Wanapozushiwa Shutuma za ajabu ajabu Kisa Wamejiunga na Chadema.

Mpaka sasa baadhi ya wanamuziki wa Bongo Fleva waliojiunga na ambao wanampango wa kujiunga na Chama Cha kuwakomboa wanyonge CHADEMA ni Afande Sele wa Morogoro, Joseph Haule ambaye anajulikana kama Prof J, Soggy Doggy na Wengineo wen

ZITTO KABWE APOKELEWA KAMA RAISI HUKO MKOAN IGOMA, ONA MWENYEWE

Mbunge wa Kigoma kaskani Mh Zitto Kabwe akisalimiana na wakazi wa Kigoma mara baada ya Kuwasili kigoma asubuhi ambapoa wakazi wa kigoma wamejitokeza kwa wingi kumpokea Mbunge wao.
Zitto Kabwe akiwa katika gari la wazi mara baada ya kutua kigoma asubuhii ambapo amepata mapokezi ya kishindo


wafuasi wa Zitto kabwe wakiwa katika maandamano..
 






















 
Support : KARIBU TENA MDADISI MAM
Copyright © 2011. RISASI - Haki Zote Zimehifadhiwa.
KWA HISANI YA MDADISI MAMBO
Proudly powered by Blogger