Search in This Blog

Showing posts with label WASANII. Show all posts
Showing posts with label WASANII. Show all posts

LAANA HIYOO YAMNYEMELEA DIAMOND

Oooh! Nooh! Wakati akimpa mama yake, Sanura Kassim ‘Sandra’ gari la Sh. milioni 38 huku akitawanya mamilioni ya fedha kwenye matukio mbalimbali, staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ anadaiwa kunyemelewa na laana kufuatia baba yake, Abdul Jumaa kuugua na kuvimba miguu bila msaada wowote.
Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akila ujana na mpenzi wake Wema Sepetu.
Kwa mujibu wa chanzo makini cha Ijumaa, baba wa staa huyo anayeishi Magomeni-Kagera jijini Dar, amekuwa akisumbuliwa na tatizo la kuvimba miguu na hakuna msaada wowote anaoupata kwani chanzo cha mapato anachokitegemea ni kodi tu ya nyumba ambayo anaipata kutoka kwa wapangaji wachache alionao.
BOFYA HAPA KUKISIKIA CHANZO
“Yaani tunashangaa kusikia Diamond ana fedha nyingi, juzikati tuliona katika gazeti kamnunulia mama yake gari la milioni 38 (Toyota Lexus-Harrier) sasa kwa nini asimthamini baba yake hata kidogo?
“Ukweli ni kwamba baba Diamond anasumbuliwa na tatizo la miguu kuvimba.

“Amekuwa akilalamika mara kwa mara lakini Diamond hatujawahi kumuona,” kilinyetisha chanzo hicho na kuongeza:“Juzikati hapa baba Diamond alishikika kwelikweli miguu, akaugulia mwenyewe ndani pasipo kuwa na msaada wowote tena nasikia mzee huyo hataki hata kuongelea lolote kuhusu Diamond maana haoni umuhimu wa kufanya hivyo wakati amemsusa muda mrefu sana.”
MATIBABU HAYAZIDI MILIONI
Katika aya nyingine, chanzo hicho kilidai kwamba ugonjwa wa miguu ambao unamsumbua mzazi huyo, gharama za matibabu haziwezi kufikia hata shilingi milioni moja za madafu achilia mbali mamilioni anayoyatapanya staa huyo.

Mama yake Diamond,Sanura Kassim ‘Sandra’ akilitesti gari alilokabiziwa na Mwanaye kama zawadi.
“Ingekuwa tatizo kubwa sana, hapo sawa, kwa sababu miguu huwa inamvimba lakini akipata dawa za kutumia huwa inarudi katika hali ya kawaida, kwa nini lakini anamfanyia hivyo baba yake? Amemkosea nini?” Kilihoji chanzo hicho.
UTAJIRI WAKE WAANIKWA
Wakati chanzo hicho kikiweka nukta hapo kwa muda, mapaparazi wetu walipewa malalamiko mengine kutoka kwa jirani mmoja wa baba Diamond ambaye alimsihi amsaidie mzazi wake kwani anaamini uwezo anao kupitia kumbukumbu ambazo Diamond mwenyewe alizithibitisha kupitia vipindi mbalimbali vya runingani kama Take One na Spora Show vya CloudsTV.

Pia kwenye vyombo vingine vya habari zikiwemo redio na magazeti pendwa ya Global Publishers.
Jirani huyo alidai kwamba mwaka jana Diamond alitangaza kuwa ana utajiri wa Sh. bilioni moja ikiaminika kwamba mwaka huu umeongezeka mara dufu.

“Nakumbuka mwaka jana kupitia Kipindi cha Spora Show na kile cha Take One, Diamond alikiri kuwa ana mkwanja usiopungua bilioni moja, hiyo ilikuwa kwa mwaka jana, sasa mwaka huu unadhani atakuwa na shilingi ngapi? Aache hizo bwana, amsaidie baba yake hata kwa kumpa mtaji mdogo wa biashara ambao unaweza kumsaidia,” alisema jirani huyo.
MATANUZI  YA DIAMOND, WEMA
Katika kuendelea kuichimba habari hiyo, mapaparazi wetu walinasa malalamiko kutoka kwa jirani mwingine wa mzazi huyo ambaye alieleza masikitiko yake kwa kulinganisha starehe ambazo staa huyo anazifanya na asali wake wa moyo, Beautiful Onyinye, Wema Isaac Sepetu na maisha halisi ya baba yake.

“Mimi ni mfuatiliaji mzuri wa habari za mastaa, naona kila siku kwenye vyombo vya habari jinsi gani Wema na Diamond wanavyotumia fedha nyingi katika masuala ambayo hayana ulazima kiivyo.
“Sisi kama majirani hatupendezwi na hali hii, angekuwa anakuja angalau siku mojamoja kumuona baba yake kuliko kila siku kumhudumia mama yake pekee,” alisema jirani huyo.

Baba yake Diamond, Abdul Jumaa akitafakari jambo.
TATIZO NI NINI?
Mapaparazi wetu waliingia mzigoni kusaka kiini halisi kwa nini Diamond amwage fedha nyingi kwa mama yake pasipo kumkumbuka japo kiduchu baba yake ambapo ilielezwa kuwa staa huyo wa Mdogomdogo hakuwa na ugomvi wowote na mzazi wake huyo.

“Kama ni ugomvi ulikuwepo kati ya mama na baba lakini Diamond hahusiki, tunashangaa kuona kama staa huyo naye anaweza kumsusia baba yake,” kilieleza chanzo na kuongeza:
“Mbaya zaidi nasikia Diamond amekuwa mzito kupokea simu za baba yake, sasa huoni kama siyo jambo la busara, mzazi ni mzazi tu hata iweje. Kwa mtazamo wangu kinachofuata ni laana.
“Kuna mifano ya watu wengi ambao waliingia kwenye laana za wazazi wao na wakajikuta kama siyo kufulia kama (wanatajwa mastaa waliofulia wa muziki Bongo) au hata kukutwa na umauti.
“Jambo hili si la kibinadamu tu, kwa wale wanaosoma vitabu vitakatifu watakuwa na mifano mingi ya watu waliowakosea wazazi wao wakalaaniwa.”

BABA DIAMOND ANASIKITISHA
Ijumaa lilipomtafuta baba Diamond kwa njia ya simu aliongea maneno ya kusikitisha huku akikataa katakata kumzungumzia kijana wake huyo.

“Jamani naomba mumuache Diamond na maisha yake, sitaki kabisa kusikia habari zake maana hata nikiongea naonekana najipendekeza kwake.
“Namshukuru Mungu, kama ni kuumwa kwa sasa naendelea vizuri na maisha yangu, niacheni nipumzike,” alisema mzee huyo kwa unyonge.
DIAMOND ANASEMAJE?
Alipotafutwa Diamond ili kumsikia anazungumziaje madai hayo, simu yake iliita bila kupokelewa. Tunaamini atasoma habari hii hivyo si vibaya akatutafuta ili afunguke kwa upande wake.

MAONI YA MHARIRI
Diamond ni staa mkubwa kwa sasa ndani na nje ya Bongo, uwezo alionao kifedha unapaswa kuendana na baraka za wazazi wa pande zote mbili. Vitabu vya Mungu vinatufundisha kwamba wazazi ndiyo Miungu wetu hapa duniani hivyo hata kama kuna kosa amefanya, mzazi atabaki kuwa mzazi tu. Hatutakiwi kumkosoa!

HII NDIYO PRIVATE JET YA MSANII JAGUAR KUTOKA KENYA TAZAMA HAPA

STEVE NYERERE AWAFUNGUKIA WANAOMZUSHIA KUWA YEYE NI SHOGA


Mwenyekiti wa bongo movie Unity, Steve Nyerere amechukizwa na watu wanaotumia mitandao vibaya na kwa kumzushia kuwa ni shoga.
Steve Nyerere kupitia akaunti yake ya facebook ameandika: Napenda kuchukua fursa hii kuongea machache na kama mtaboa mtu naomba samahani najua binadamu tumezaliwa tofauti sana kuna wale wanaogopa zambi na kunawale wanopenda zambi mimi daima nasema izo ni changamoto tuuu ok nimepata taarifa umu umu kwenye mitandao yetu ya kijamiii hususani huuu kwamba kuna binti anaitwa zainab ananichafua na kuniandika mambo ambayo ayana tija kwangu. 
Nazani ata kwake kwamba mimi shoga anauhakika hahahahaha nimecheka sana kupata izi taarifa nataka kuwapa taarifa ndugu zangu kuna msemo unasema mti wenye matunda ndio unaopigwa mawe na mkanya mara moja aache mara moja kwani naimani anapoteza muda tu habari hizo si zakweli kabisa ila namtakia laheli kwahili jambo analonitendea mimi nasema namwachia mola akumbuke nafamily mke na watoto mama dada zangu kiukweli najisikia vibaya sana mi nasema asante”.
Baada ya kuandika kauli hiyo, Steve Nyerere ameuambia mtandao wa bongo5 kuwa kuna watu wameamua kumchufua baada ya kujionyesha wazi kwenye siasa.

Watu wananitumia meseji mbaya, eti mimi nimetumwa na viongozi, mara sijui mimi ni shoga, jamani hakuna mambo kama hayo, nawataka watanzania wajue hayo ni mambo za uzushi, sijui ata yametoka wapi Alisema Steve Nyerere

JACKLINE WOLPER AFUNGUKA YOTE KUHUSU YEYE NA NEY WAMITEGO SOMA HAPA KUJUA ALICHOSEMA PATA STORI HAPA

Huko Instagram kuna Jamaa Anajiita Dougiemasta13 sijui Siwema ambae ni mchumba wa Nay wa Mitego kamkosea nini Maana madogo anayomshushia...Duuuhhh ...Baada ya Jana Kuweka Video ya Wema akivishwa pete na Jamaa mwingine leo Kaja na Mpya....


JIONEEE..... 


FLORA MBASHA NA MUMEWE BADO NDOA YAO IPO KATIKA VURUGU KUBWA

Imebainika  kwamba  waimbaji  wa  muziki  wa  Injili  nchini, Flora Mbasha  na  mumewe, Emmanuel  Mbasha  hawajapatana  kama ilivyodaiwa  awali  na  taarifa  zinasema  kuwa  mwanadada  huyo  ameanza  maisha  yake  kivyake  kwa  kupanga  nyumba  nyingine  mbali  na  mumewe….
 
Habari  za  kuaminika  toka  ndani  ya  familia  ya  Flora  zinasema  kuwa  msanii  huyo  amekuwa  na  wakati mgumu  wa  kumsamehe  mumewe  kutokana  na  tabia  zake  chafu  ambazo  zimekuwa  zikiutesa  moyo  wake  na  sasa  anang’ang’ania  kumchukua  mwanaye…..
 
“Hivi  karibuni  iliripotiwa  kuwa  wanandoa  hao  wamepatana  lakini  ukweli  ni  kwamba  hakuna  kitu  kama hicho,mwanamke  amepanga  chumba  chake  hapa  Dar  es  Salaam  na  kumwachia  kila  kitu  mumewe  ambaye  sasa  ana haha  kumchukua  mwanaye  ili  aishi  naye,” kilisema  chanzo  cha  habari.
 
Lakini  upande  wa  pili, mume  wa  msanii  huyo  hivi  karibuni  alieleza  kuwa  ugomvi  baina  yao  ulianza  kutokana  na  kuchepuka  kwa  mkewe, huku  akipeleka  shutuma  kwa  mchungaji  wa  kanisa  la  ufufuo  na  Uzima, Josephat  Gwajima  ambaye  ni  maarufu  kwa  vitu  ambavyo  ni  tofauti  na  huduma  zake….
mbasha
Emmanuel  Mbasha  tayari  alishatoa  waraka  wa  wazi  kwenda  kwa  mchungaji  huyo, akimtaka  kukaa  mbali  na  ndoa  yake  jambo  ambalo  bado  halina  mrejesho  chanya  kwani  wawili  hao  Flora  na  Gwajima  wameendelea  kufanya  kazi  pamoja  kitu  kinachopelekea  Emmanuel  kuona  bado  kuna  kitu  kinaendelea  kati  yao….
 
Kutokana  na  hali  hiyo, mume  wa  Flora  amekuwa  mgumu  kumtoa  mtoto  wake  akihofia  kulelewa  na  mtu  ambaye  kwake  anamchukulia  kama  adui  wa  familia  yake…
 
“Imekuwa  ngumu  sana  kwa  Emmanuel  kumwachia  mtoto  wake  katika  hali  hii, hata  kama  ni  wewe  unamuachiaje  mtoto  wako  kipenzi  aende  kwa  mwanamke  ambaye  ni  msaliti,” alisema  ndugu  wa  karibu  wa  Emmanuel  Mbasha

MARTIN KADINDA AFUNGUA NA KUELEZA UKWELI KAMA YEYE NI SHOGA AU LA, TWENDE PAMOJA HAPA

Mbunifu wa mavazi nchini, Martin Kadinda amesema kuwa amekuwa akikutana na changamoto kutoka kwa wanaume wengi wanaodhani kuwa yeye ni shoga na kufikia hatua ya kumtumia ujumbe wa kumtaka kimapenzi.
“Kila mtu anakuwa na maswali yake anaya-raise kutokana na anacho kifikiria katika akili yake, Watanzania tunatabia ya ku-create situation katika akili zetu halafu we want everybody to accept.Kwamba mtu tu anaamka asubuhi may be ana matamanio na wewe anaanza ku-raise hilo swali aone jibu litakuwa ni nini. Wapo wengi (wananitamani) wako hivyo, facebook, Instagram mtu atakutumia namba yake, hakwambii lakini unaona kabisa huyu, nakukubali sana I wish siku moja uje nyumbani kwangu au can I come to your place, mimi sitakagi hata kwenda huko najua nitajiuliza imekuaje mpaka imefikia hivi, basi nasema sawa. Kwa sababu mimi facebook nakuwa mkweli sijawahi kujibu mtu tangu 2012, I have a person huwa anazipitia, akiulizia mtu maswala modelling mpe namba ya fulani, mambo mengine binafsi usiwajibu achana nao, kwa sababu mara ya kwanza nilikuwa ninadhani I should meet these people talk to them this is not right but nikaona unapoanza kuwa unajihusisha ndipo unapojikuta unaanza kuingia bila kujua” Martin Kadinda aliambia Sporah Show.
kadinda
Pia Martin amesema kuwa ana mpenzi wake ambaye hapendi kumuweka wazi ili kulinda heshima yake.
“Ukishakuwa maarufu na mtu wa karibu yako atakuwa maarufu, she’s not already kwa hiyo kitu yakuingia kwenye hiyo cycle kila siku wanamuona kwenye magazeti kwenye Instagram haiko hivyo. Ndiyo maana hata nikiweka picha yake Instagram nitaweka picha yake moja kwa miezi sita, yupo hata ukitaka kumuona kwenye Instagram yangu yupo, first lady wa martin huyu, lakini cycle yake na maisha yake siyo mtu wa kukaa kwenye media nadhani ni kwa sababu ya future ya kazi atayokuja kuifanya kwaiyo anajitaidi kuwa pembeni… Mara ya kwanza alishawahi kuniuliza alipita kwenye comment za watu kwenye blog fulani akasoma, akaniambia najua hii ni Watanzania walivyo, as long nakutambua mwanaume wangu ni mtu wa namna gani I don’t care about these people” Alimaliza Martin

HAPPYNESS MAGESE ANAHALI MBAYA SANA, SASA AKOJOA KWA KUTUMIA MIPIRA

Happiness Magese anasihi wanawake kucheki afya zao mara kwa mara wasije wakakutwa na tatizo kama lake la ugumba ambalo limeharibu na kibofu chake na kupelekea hata kushindwa kukojoa kwa njia ya kawaida na badala yake anatumia mipira, ni vema kuchek afya mara kwa mara.
magesa

HIVI NDIVYO WEMA NA DIAMOND WALIVYOKUTANA SIKU YA KWANZA

Screen Shot 2014-03-28 at 1.52.37 AM

Screen Shot 2014-03-28 at 4.07.47 AMInaaminika katika mapenzi au uhusiano wa kimapenzi uliowahi kuandikwa sana kwenye mitandao na magazeti Tanzania, huu wa mwigizaji Wema Sepetu na Diamond Platnumz umevunja rekodi, mastaa ambao walifikia mpaka kuvalishana pete ya uchumba.

Pamoja na yote waliyopitia bado kalamu za Waandishi mbalimbali zilihusika kuwaandika.
Ommy Dimpoz ambae ni rafiki wa Diamond kitambo hata kabla hatawa staa (Ommy) ameshea hii picha inayowaonyesha Wema na Diamond walipokutana kwa mara ya kwanza na kuiambatanisha na hii caption hapa chini.
Screen Shot 2014-03-28 at 1.52.48 AM

HII NDIO HEKAHEKA INAYOMHUSU MAMA WA DIAMOND PLATNUMZ

mama diamondMama yake Diamond Platnumz leo July 11 alikua kwenye kipindi cha Leo Tena kutoka Clouds Fm na alipata nafasi ya kutoa Hekaheka yake ambayo inahusu maisha yake pamoja na Diamond Platnumz kwenye malezi yake mpaka hapo alipo Diamond kwa sasa. dmn

JAMAA ANAVYOMFAIDI WEMA, LAITI KAMA DIAMOND ANGEMFUMA... MMMH SIJUI INGEKUWAJE



 Wema Sepetu na Kajala wakibadilishana mawazo huku burudani ya Skylight Band ikiendelea.
 Benny Kinyaiya, William Malecela na Wema Sepetu.
 Pichani juu na chini ni Wema Sepetu akimpagawisha Sam Mapenzi wa Skylight Band 
 Sam Mapenzi akimwimbia Wema Sepetu ndani kiota cha Thai Village kilichopo Masaki jijini Dar Juma lililopita.
Maimatha wa Jesse akishow love na marafiki alipotinga kwenye kiota cha Thai Village kuanza week end yake na burudani za Skylight Band
Aneth Kushaba AK47 na Mary Lucos wakitoa burudani kwa mashabiki wa Skylight Band.

RAY C APIGWA VIBAYA NA CHID BENZI

evu! Rapa mwenye ‘swagger’ za Ja-Rule Bongo, Rashid Makwilo ‘Chid Benz’, anadaiwa kukwaa kisanga kingine kibaya baada ya kukurupuka kutoka nyumbani kwake na kwenda kumvamia staa mwenzake, Rehema Chalamila ‘Ray C’ nyumbani kwake anapoishi na kumtwanga makonde ikiwa ni siku chache tangu jamaa huyo apate msala mwigine wa aina hiyo.
Rapa mwenye ‘swagger’ za Ja-Rule Bongo, Rashid Makwilo ‘Chid Benz’.
TUJIUNGE NYUMBANI KWA RAY C
Ilidaiwa kuwa tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia Alhamisi iliyopita nyumbani kwa Ray C, Changanyikeni jijini Dar es Salaam ambapo ilisemekana kwamba Chid Benz alimvamia mishale ya saa 4:00 usiku kwa gia ya kumsaka mzazi mwenzake aliyemtaja kwa jina moja la Mariam.
Mwanaisha aliyepigwa na Chidi Benz hapo awali.
CHID BENZ ATAKA KUMUONA MWANAYE
Ilidaiwa kwamba Chid Benz alisema kuwa alizungumza na mpenziye huyo kwamba alitaka kwenda kumuona mwanaye ambapo Mariam alimjibu kwamba kwa muda huo alikuwa nyumbani kwa Ray C  Changanyikeni.
UNGA WATAJWA
Sosi wetu alidai kwamba baada ya kujibiwa hivyo, Chid Benz alianza kulalama na kumwambia anamfuata palepale kwa nini usiku ule alale kwa Ray C, wakati ana uwezo wa kwenda nyumbani au amekwenda kwa staa huyo ili kunywa dawa zao za kuondoa sumu ya madawa ya kulevya ‘unga’, jambo ambalo jamaa huyo siku zote huwa hataki hata kulisikia masikioni mwake.
Staa wa muziki wa Bongo Fleva, Rehema Chalamila ‘Ray C’.
CHID BENZ AWAVAMIA
“Huwezi kuamini baada ya muda kama wa saa moja, Ray C na Mariam wakiwa ndani wakitazama TV, ghafla mlango ulisukumwa kwa nguvu kisha akaingia Chid Benz na kumdaka Mariam na kuanza kumshushia kipigo.“Yaani huo mshtuko walioupata walidhani wamevamiwa na Al-Shabaab.
KIBAO CHAMGEUKIA RAY C
“Mungu mkubwa kwa sababu Mariam alifanikiwa kuchoropoka na kukimbilia chumbani ndipo kibao kikamgeukia Ray C.
Sehemu ya damu chumbani kwa Ray C kutokana na kipigo cha Chidi Benz..
“Ray C akiwa anashangaa ghafla naye alipokea kipigo kikali kutoka kwa Chid na kumsababishia majeraha mbalimbali mwilini.
RAY C AKIMBILIA KWA MAJIRANI
“Baada ya kuona maji yanazidi unga, Ray C alitafuta upenyo na kukimbilia kwa majirani huku akipiga kelele za kuvamiwa, mara moja majirani waliambatana naye mpaka nyumbani kwake.
“Walipofika Chid Benz alikuwa ametumia staili za kininja kwa kuruka geti na kutokomea kusikojulikana huku akiwaacha Ray C na Mariam wakiangua vilio kwa kipigo kikali walichopokea.
RAY C AVUJA DAMU
“Ray C aliumia mkono na mguu ambao ulionekana ukivuja damu. Mariam alikuwa akililia mbavu zake kuchakazwa kwa makonde mazito na upande mwingine baadhi ya vyombo vya ndani vikionekana kuvunjwa na vingine kusambaratishwa kufuatia tafrani iliyozuka muda mfupi baada ya Chid Benz kutia maguu nyumbani hapo,” chanzo kilishusha madai hayo mazito.
RAY C ATIRIRIKA SAKATA LILIVYOKUWA
Akizungumzia na gazeti hili Alhamisi iliyopita juu ya sakata hilo, Ray C alisimulia mkasa mzima: “Kweli Chid Benz alikuja nyumbani kwangu na kunivamia.
“Alinipiga vibaya sana na kuvunja baadhi ya vitu vya ndani kwangu, jambo ambalo lilinishangaza zaidi ni namna alivyopafahamu nyumbani kwangu hadi kuja kunifanyia fujo nikiwa na mzazi mwenzake, Mariam ambaye nilitoka naye ofisini kwangu.
“Ujue jana (Jumatano) tulikuwa na kazi sana ofisini kwangu mimi na Mariam, sasa kutokana na kubanwa na kazi kweli muda ulienda sana hivyo nikamwambia Mariam akalale kwangu.
“Kwa kuwa muda ule ilikuwa ngumu kwenda kwao Mbezi Beach, Mariam alikubali na tulikwenda wote nyumbani kwangu.
“Huko nyuma Mariam alikuwa mwathirika wa madawa ya kulevya lakini baada ya kusikia mimi nimeacha, naye aliachana nayo na kuanza kutumia dawa za kuondoa sumu.
“Tumeendelea kutumia naye dawa na sasa ameshapona kabisa hivyo kuna baadhi ya kazi nimekuwa nikimshirikisha kunisaidia kwenye ofisi yangu. Pia alishawahi kumshawishi Chid Benz ili aje kutumia dawa lakini jamaa alikataa na kumfanyia vurugu sana huku akimkataza kuwa na mimi kwa madai mimi ndiyo namfanya amwambie kuachana na utumiaji dawa za kulevya.
“Sasa jana alipojua hivyo nadhani Chid Benz alikuja kutimiza dhamira yake ambayo siku nyingi alikuwa akiahidi kunipiga.”
SOO LIPO POLISI
Ray C alisema baada ya tukio hilo alikwenda kuripoti kwenye Kituo cha Polisi cha Oysterbay, Kinondoni na kufunguliwa jalada la kesi ambapo Chid Benz anasakwa na polisi.
Juhudi za kumpata Chid Benz hazikuzaa matunda kwani simu yake haikuwa hewani hivyo jitihada zinaendelea na kama ana ufafanuzi au utetezi anaweza kutupigia.
CHID BENZ NI TATIZO?
Chid Benz anadaiwa kuwa ni tatizo kwani tukio hilo la Ray C amelifanya wakati akiwa na tukio la pili kwa wanawake kwani kwenye Mahakama ya Mwanzo, Ilala ana kesi mbichi aliyoshitakiwa kwa kosa la kumpiga mrembo aitwaye Mwanaisha.
Mbali matukio hayo pia Chid Benz ana rekodi ya kukorofishana na wasanii wenzake kama Kalapina na marehemu Ngwea.

KWELI JINI KABULA NI MALAYA WAKUTUPWA, ANGALIA USHENZI ALIOSEMA KUHUSU MWEZI MTUKUFU WA RAMADHANI NA VIMINI VYAKE

STAA wa sinema za Kibongo, Miriam Mjolwa ‘Jini Kabula’ amecharuka baada ya kukosolewa juu ya mavazi ya mitego, vimini, anayovaa ndani ya mwezi wa Ramadhani.
Staa wa sinema za Kibongo, Miriam Mjolwa ‘Jini Kabula’
Baada ya majirani wanaofunga kufikisha malalamiko, paparazi wetu alimvutia waya Jini Kabula na kumsomea mashtaka hayo ambapo alisema kuwa alikuwa lokesheni siku waliyomuona lakini pia hahofii sana kwani mwezi huo haumuhusu.
“Hao wanaweka chumvi tu mimi sikuwepo huko mtaani nilikuwa lokesheni tangu mwezi uanze, na hata kama nitavaa nguo za ajabu, mwezi huu haunihusu nitavaa vyovyote nipendavyo,” alisema Jini Kabula.

KAJALA: WEMA NI MNAFIKI NA PIA NI KIGEUGEU


Musa Mateja na Shakoor Jongo STAA wa filamu za Kibongo, Kajala Masanja ameibuka na kusema kuwa ushosti wake na Miss Tanzania 2006/07, Wema Sepetu, uliorudishwa hivi karibuni baada ya kuwekana sawa ni wa kinafiki huku akidai Wema ni kigeugeu.
Staa wa filamu za Kibongo, Kajala Masanja
Akizungumza kwa kujiamini mbele ya waandishi wetu, juzi Jumatano pande wa Mikocheni jijini Dar es Salaam, Kajala alisema: “Wema ni mnafiki kabisa. Upatanisho wetu ni wa uongo. Mimi moyoni nimeondoa kinyongo lakini mwenzangu naona kama bado ana donge moyoni.”
Kajala alisema hayo alipoulizwa na Risasi Jumamosi, sababu ya kutoonekana kwenye tukio la futari lililofanyika nyumbani kwa mama mzazi wa Mbongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Sanura Kassim ambaye ni mkwe wa shosti wake huyo.
Katika tukio hilo, mama Diamond alifanyiwa sapraizi ya nguvu alipokabidhiwa gari kali aina ya Toyota Lexus Harrier kama zawadi ya bethidei yake, ambayo ilitolewa na meneja wa Diamond, Babu Tale kwa niaba ya mwanamuziki huyo ambaye alikuwa safarini nchini Marekani.
Miss Tanzania 2006/07, Wema Sepetu,
“Tunakubaliana kuwa kitu kimoja lakini mwenzangu anaonekana ana kinyongo. Hebu angalia, anawezaje kuacha kunialika kwenye shughuli muhimu kama ile kama kweli tumepatana? Mbona amealika watu wengi lakini mimi ameniacha? Wema aache unafiki bwana.
“Mbaya zaidi, hivi juzi tu ameweka picha ya msichana mmoja anayekaa China, huyu mdada anaitwa Sabrina, niliwahi kugomabana naye, lakini yeye amemuweka Instagram na kumwandikia maneno kibao ya kumsifia akim-wish happy birthday, hapo si kama ananisimanga? Wema si mkweli,” alisema Kajala.
Akizungumzia ishu hiyo, siku ya tukio Wema alisema: “Ukiniuliza kuhusu Kajala kutokuwepo hapa, kwa kweli utakuwa kama unanichanganya tu maana leo sijashika simu muda mrefu sana.
“Hata ujio wangu hapa nilikurupushwa, ndiyo maana sijakumbuka kumuita Kajala, lakini tuko vizuri na mara ya mwisho tumeongea jana (Jumapili) usiku tu,” alisema Wema.

MZIMU WA RECHO WAZIDI KUWATESA WASANII, SSA NI ZAMU YA SAGUDA

Stori: Erick Evarist
WAKATI Arobaini ikitarajia kufanyika jana, mchumba wa marehemu Sheila Haule ‘Recho’, George Saguda ameeleza kuwa bado aliyekuwa mchumba wake huyo anamtesa kwa kumtokea mara kwa mara.
Marehemu Sheila Haule ‘Recho’, akiwa na mpenzi wake George Saguda enzi za uhai wake.
Akizungumza na mwanahabari wetu, Saguda alisema marehemu amekuwa akimtokea akiwa usingizini na kumsisitiza kuhusu kazi.“Najitahidi sana kuondoa mawazo juu yake lakini bado ananitokea, sijui hali hii itaisha lini,” alisema Saguda.
Recho kabla hajapatwa na umauti, walizalisha filamu mbili katika kampuni yao ya Sara Entertainment ambazo ni Vanessa na Fedheha ambayo imetoka hivi karibuni.

MFUNGO WAMBADILI JOHARI MAVAZI, MWEZI HUU HAVAI TENA VIMINI

MWIGIZAJI wa filamu Bongo, Blandina Chagula ‘Johari’ amesema amewaunga mkono Waislamu kwa kuvaa mavazi ya kujistiri na kuziba sehemu kubwa ya mwili kuheshimu mwezi wa Ramadhani.
Mwigizaji wa filamu Bongo, Blandina Chagula ‘Johari’.
Akipiga stori mbili tatu na paparazi wetu, Johari alisema ameamua kufanya hivyo kwa sababu dini zote ni za Mungu na kwa kuwa ni kipindi cha Ramadhani, amebadilika kwa kila kitu.
“Kipindi hiki ni cha kumrudia Mungu, nimeacha kila kitu kibaya kwa kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhani na nimeamua kutulia ili nipate muda mwingi wa kuomba,” alisema Johari.

DIAMOND NI MWIZI, KANIIBIA WIMBO WANGU, HAYA NI MAENO YA WABABA

 Malalamiko ya wasanii kuibiana au kupigana kanzu kwenye kazi zao yaliripotiwa sana mwaka jana na mwaka huu mambo yalikuwa shwari, lakini baada ya kuvuka nusu ya mwaka yameibuka tena.
Mshiriki wa shindano la kuimba la Bongo Star Search (BSS) , Wababa amewatuhumu maswaiba wa ‘Muziki Gani’ Nay wa Mitego na Diamond Platinumz kwa kumuibia kazi zake kwa wakati tofauti. 

Akiongea kupitia Friday Night Live ya East Africa TV, Wababa amesema Diamond amemuibia wimbo wake ambao alikua anaiita ‘Kitorondo’ na kwamba aliibadilisha jina baadae.
Kiukweli kuhusu Diamond, mimi mwenyewe nimetumiwa hiyo ngoma ambayo ameitoa, nimeiskiliza jinsi ilivyo kuanzia idea, mwendo, style ambazo anafanya. Ambayo ameibadilisha jina tu baada ya ya kwamba ilikuwa mitandaoni nilikuwa nimemfatilia ilikuwa inaitwa Kitorondo mwezi mmoja kama uliopita. Kwa hiyo nilishindwa kulalamika kwa sababu yeye mwenyewe alikuwa analalamika kuwa imevuja. Kwa hiyo sikuona sababu ya kuongea kitu kwa sababu haikuwa official. Kwa hiyo sikuwa na sababu ya kucomplaini kwa sababu haikuwa official, lakini mpaka jana ina maana ilikuwa serious kama biashara.” Ameeleza Wababa.
                                                                        Wababa 
 Alipoulizwa ni wapi ambapo Diamond aliusikia wimbo huo, amesema huo ni wimbo wake alioutoa miaka minne iliyopita akiwa na Dogo Asley na aliuweka kwenye mtandao wakati anatumia jina la Nurdi, kabla hajaanza kutumia jina la Wababa aliposhiriki BSS. “Ni nyimbo ambayo iko mtaani na watu wengi wanaielewa. Kwa hiyo sijaelewa..” Kwa upande mwingine, Wababa amedai kuwa alifanya kazi na Nay wa Mitego katika studio za Mazoo lakini baaadae Nay alirudi studio na kuongea na Mazoo kutaka kuunua wimbo huo kwa shilingi milioni  moja bila kumshirikisha Wababa.
Hivi karibuni nimefanya ngoma mpya na Nay wa Mitego, ni ngoma ambayo ilikuwa iko paid kwake pamoja na studio. Lakini kitu cha kushangaza ni kwamba siku mbili baada ya kufanya kazi nikapigiwa simu na producer akaniambia kwamba jamaa amerudi tena kwa ajili ya kutaka kununua wimbo kwa milioni moja, auchukue wimbo aende akaufanye sehemu nyingine. Baada ya hapo hata mahusiano yangu na mshikaji yamekuwa sio mazuri. Ukimpigia simu anakwambia yuko busy kuna kazi anafanya atanicheki, hadi kufikia leo sielewi.”
Nay alipigiwa simu lakini hakuwa anapatikana kwa muda huo.

UWOYA NA MASOGANGE WANAISHI PAMOJA SOUTH, JE KUNANII?


Hili ni swala la kujiuliza...ingawa hadi sasa Uwoya hajasema chochote...Lakini Masogange kupitia ukurasa wake wa INSTAGRAM amekuwa akiweka picha kadhaa za Irene Uwoya wakiwa pamoja huko SAUZI....Sasa katika kumaliza zaidi jana ameka video Irene akiwa anapika....HEHEHEHE

PICHA ZA AGNES MASOGANGE AKIWA NA NJEMBA YAKE KUTOKA SOUTH AFRIKA

SIRI YAFICHUKA, WEMA NA DIAMONDA SASA NI ......

http://photos-g.ak.instagram.com/hphotos-ak-xpa1/927739_312353152262798_239351557_n.jpg

IN THE NAME OF #INSTAGRAM
 ONE OF WEMA'S FAN COME WITH A DOUBT CONCERNING A RING WHICH SEEMED ON THE WEMA'S COURT FINGER SO THE QUESTION COMES DOES WEMA SEPETU TAKE IT FOR DECORATION OR NEAR TO MARRIAGE??

POWER TO YOU!!

ONE OF WEMA'S FAN COME WITH A DOUBT CONCERNING A RING WHICH SEEMED ON THE WEMA'S COURT FINGER SO THE QUESTION COMES DOES WEMA SEPETU TAKE IT FOR DECORATION OR NEAR TO MARRIAGE?? POWER TO YOU!!

WASTARA: NIMEGUNDUA WANAUME WENGI WANATAKA KUNIVUA CHUPI TU

Msanii wa filamu Bongo, Wastara Juma amefunguka kuwa tangu mume wake Juma Kilowoko ‘Sajuki’ afariki dunia, wamekuwa wakijitokeza wanaume kibao wakitaka kumuoa lakini amegundua wengi wana nia ya kunitumia tu.
Msanii wa filamu Bongo, Wastara Juma.
Akizungumza na mwandishi wetu hivi karibuni, Wastara alisema kama mwanamke amekuwa akitamani kumpata mwanaume wa kumfariji lakini kinachomchanganya ni sampuli ya wanaume wanaotuma maombi kwake.
“Mpaka sasa wameshanitokea wanaume zaidi ya kumi lakini wengi wao nawaona wananitaka ili kujua nini nilichonacho na wengine wananifuata wakidhani watapata mali na si mapenzi ya dhati.
“Kimsingi wanataka tu kujua Sajuki alidata na nini kwangu, mimi siko hivyo. Siwezi kumruhusu mtu aingie kwenye maisha yangu kwa masilahi yake. Ninayemhitaji namjua moyoni na ipo siku nitampata kwani siangalii mfuko wa mtu, naangalia tabia,” alisema Wastara.
 
Support : KARIBU TENA MDADISI MAM
Copyright © 2011. RISASI - Haki Zote Zimehifadhiwa.
KWA HISANI YA MDADISI MAMBO
Proudly powered by Blogger