Ama kweli dunia haina huruma! Dada Happy amejikuta akiishiwa nguvu na kuanguka mbele ya kadamnasi na kuzimia pasipo msaada wowote ambapo badala yake watu waliodaiwa kuwa ni vibaka walimuibia vitu vyake vyote.
Ilidaiwa kuwa baada ya kupoteza fahamu, wahuni walimliza simu pamoja na fedha zote kisha kumwacha akiwa hana msaada wowote.
Gazeti hili lilitaka kujua kilichompata mrembo huyo lakini madaktari hospitalini hapo walidai hawawezi kutoa siri ya mgonjwa huku ndugu nao wakiweka ngumu kusema kilichosababisha Happy kudondoka ghafla na kupoteza fahamu.