Bodi ya Ukaguzi wa Filamu na Michezo ya Kuigiza Tanzania, imeagiza kuwa filamu ya marehemu Steven Kanumba 'Love&Power' inayotarajiwa kuingia sokoni rasmi leo, inatakiwa kuangalia na watu wenye umri wa kuanzia miaka 16 na kuendelea.
Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu nchini Joyce 
Fisoo aliagiza umri wa kutazama filamu ya Love & Power ni miaka 16 
na kuendelea.
                
              
"Baada ya kuikagua filamu hii tumependekeza umri 
stahiki wa kutazama filamu hii ambao ni kuanzia umri wa miaka 16," 
alisema Fisoo.
                
              
Akizungumza Msemaji wa filamu hiyo Myovela Mfwaisa
 alisema Love&Power ni filamu nzuri inayotazamwa na watoto pamoja na
 familia, iliyopewa kibali cha ukaguzi Kutoka Bodi ya ukaguzi wa filamu 
na michezo ya kuigiza Tanzania.
                
              
"Lugha iliyotumika katika filamu hiyo ni Kiswahili lakini pia Lugha ya kiingereza imetumika kama ‘Subtitles’. "
                
              
“Filamu ya Love & Power imetengenezwa na 
kampuni ya Kanumba the Great film kwa kushirikia na Steps Entertainment 
Ltd ikiwa imeandikwa na Ally Yakuti, Filamu ya Love & Power 
imeshirikisha wasanii nyota katika tasnia ya Filamu Tanzania kama 
Hussein Mkiety ‘Sharomilionea’, Irene Paul, Patcho Mwamba, Grace 
Mapunda, Hartman, Rammy Galis pamoja Seth Bosco ambaye ni mdogo wake na 
marehemu na kuongozwa na Steven Kanumba."
                
              
Alisema watayarishaji wakuu ni Steps Entertainment Ltd na pia imetengenezwa  jijini Dar es Salaam katika maeneo tofauti tofauti.
                
              
 Myovela aliwaomba wasanii kuwa walinzi wa kazi hiyo ya marehemu kwa kupambana na maharamia wa kazi za Wasanii wa filamu.
                
              
 "Tunawaomba wapenzi wa filamu kununua nakala 
halali yenye nembo ya Steps Entertainment Ltd, hiyo itachochea maslahi 
kwa wasanii wa Tanzania na kuongeza ajira kwa vijana ili kufikia hilo 
nunua filamu ya Love & Power halali." alisema Myovela.
No comments:
Post a Comment