
Akipiga stori na paparazi wetu, Mainda alisema ameamua kuacha kutumia mkorogo kutokana na matakwa ya dini yake, amegundua anamkosea Mungu wake kwa kujichubua
.
“Nimeamua tu kuacha kujichubua, mkorogo siyo kitu kizuri hata Mungu hapendi vitu hivi ndiyo maana nikaamua kuuacha japo nimetumia kwa muda mrefu,” alisema Mainda ambaye kabla ya kuokoka alikuwa Muislamu.